MKURUGENZI WA TIBA WIZARA YA AFYA APONGEZA UBORESHAJI HUDUMA ZA DIALYSIS KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MWANANYAMALA
Posted on: August 1st, 2023Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara ya Afya Prof. Paschal Ruggajo ameupongeza uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwananyamala kwa kuhakikisha huduma za Dialysis zinatolewa kwa ubora na viwango vinavyotakiwa.
Prof. Ruggajo ameyasema hayo leo alipofanya ziara katika Hospitali hiyo yenye lengo la kukagua huduma zinazotolewa na Kitengo cha Dialysis na uwezo wake wa kutoa huduma hizo ambapo amekiri kuridhishwa na utoaji huduma unaofanywa na Kitengo hicho.
Nchi yetu imepiga hatua kubwa katika Ukanda wa Afrika Mashariki katika utoaji wa huduma za Dialysis, nimeridhika sana na huduma zitolewazo hapa na niseme tu Mwananyamala ya sasa si ya zamani.